Napaswa kujua nini kuhusu kondomu za wanaume

From Audiopedia - Accessible Learning for All
Jump to: navigation, search
QR for this page

https://www.audiopedia.org/Napaswa_kujua_nini_kuhusu_kondomu_za_wanaume

Kondomu ya wanaume ni mfuko mwembamba wa mpira ambao mwanaume huvaa kwenye uume wake kabla ya kushiriki ngono. Kwa sababu shahawa inakaa ndani ya mfuko, mbegu haziwezi kuingia katika mwili wa mwanamke.

Kondomu hutoa kinga kamili kutokana na mimba. Kinga hii huwa madhubuti ikiwa kondomu itatumika pamoja na dawa ya kuua mbegu na mafuta yanayotumika kurahisisha tendo la ngono.

Kondomu hazina madhara yoyote. Kondomu ni kinga bora dhidi ya magonjwa ya zinaa na virusi vya HIV. Kondomu zinaweza kutumika pekee au pamoja na njia nyingine ya kupanga uzazi. Kondomu zinaweza kununuliwa katika maduka ya madawa, na pia zinapatikana katika vituo vya afya na katika warsha za kuzuia UKIMWI.

Ni lazima kondomu ivaliwe wakati uume umesisimka, lakini kabla ya kugusa sehemu ya mwanamke ya siri. Ikiwa uume wake utagusa sehemu za mwanamke za siri au kuingia kwenye uuke, basi mwanamke atashika mimba au kuambukizwa magonjwa ya zinaa, hata kama hatamwaga shahawa (ejaculate).

Ikiwa kondomu itapasuka au kutoka kwenye uume, itabidi mwanamke aweke dawa ya kuua mbegu ndani ya uuke wake mara moja. Ikiwezekana, tumia mbinu ya mpango wa uzazi ya dharura.

Kumbuka:

  • Tumia kondomu kila unaposhiriki ngono.
  • Mwanamke anayetumia mbinu nyingine ya kupanga uzazi lazima pia atumie kondomu ili kujikinga kutokana na magonjwa ya zinaa.
  • Ikiwezekana, tumia kondomu zilizotengenezwa kwa latex. Kondomu aina hii hutoa kinga kamili kutokana na UKIMWI. Kondomu zilizotengenezwa kwa ngozi ya kondoo au mbuzi hazitakukinga kutokana na virusi vya HIV.
  • Weka kondomu mahali pakavu, mbali na miale ya jua. Ni rahisi kwa kondomu zilizoko kwenye pakiti nzee na zilizoraruka kupasuka.
  • Tumia kondomu mara moja tu. Kondomu ambayo imeshatumika inaweza kupasuka.
  • Weka kondomu mahali ambapo unaweza kuzifikia. Ni rahisi kukosa kuzitumia ikiwa utasimamisha shughuli ili kuzitafuta.
  • Pale mwanzoni, wapendanao hawapendi kutumia kondomu. Wanapozoea, huweza kugundua faida zake, zaidi ya kukinga kutokana na mimba zisizotakikana na magonjwa ya zinaa. Kwa mfano, kondomu huwasaidia baadhi ya wanaume kusitisha kumwaga shahawa.
  • Tahadhari sana usirarue kondomu/mpira wakati unaporarua pakiti yake. Usitumie kondomu mpya ambayo pakiti yake imeraruka au kukauka, au ikiwa kondomu yenyewe inanata au ni ngumu. Kondomu hiyo haitafanya kazi. Usiifungue kondomu kabla ya kuivaa.
Sources
  • Burns, A. A., Niemann, S., Lovich, R., Maxwell, J., & Shapiro, K. (2014). Where women have no doctor: A health guide for women. Hesperian Foundation.
  • Audiopedia ID: sw020410