Nawezaje kuzuia kupata mimba kwa kunyonyesha katika miezi 6 ya kwanza
From Audiopedia - Accessible Learning for All
QR for this page
Kunyonyesha kunaweza kuzuia mwili kutengeneza yai. Mbinu hii haina gharama yoyote, lakini inaweza kutumika tu katika miezi 6 baada ya kujifungua pekee.
Kunyonyesha ni mbinu mwafaka ya kupanga uzazi, lakini sharti mambo yafuatayo yazingatiwe:
1. Mtoto wako yuko na umri wa chini ya miezi 6.
2. Haujapata hedhi tangu kujifungua.
3. Unamnyonyesha tu mtoto wako, na hii ni kila mara anapohisi njaa, usiku na mchana, na haupitishi masaa 6 kabla hujamnyonyesha. Mtoto wako halali usiku kucha bila kunyonya.