Nifanyeje ikiwa mtu katika familia yangu anataka kushiriki ngono na mimi
From Audiopedia - Accessible Learning for All
QR for this page
Sio sawa kwa mtu kukushika ikiwa wewe hutaki kushikwa. Watu wa familia moja kama vile binamu, mjomba, ndugu au baba, hawafai kushika sehemu zako za siri au sehemu yoyote ya mwili wako kuashiria kujamiiana.
Tafuta usaidizi ikiwa hili litafanyika.
Hata kama mwanaume huyo atakuambia kuwa atakudhuru ukimshtaki, lazima umwambie mtu ambaye unamwamini haraka iwezekanavyo. Wakati mwingine ni vyema kumwambia mtu ambaye sio wa familia yako, kama vile mwalimu wako wa kike au kiongozi wa kidini katika eneo lako.